Uhusiano wa China na Afrika Mashariki kama Ilivyobainishwa katika Fasihi ya Kiswahili

Authors

  • Wael N.I. Othman Chuo Kikuu cha Al-Azhar

Abstract

Makala hii inalenga kuangazia uhusiano wa China na Afrika Mashariki kama ilivyobainishwa katika fasihi ya Kiswahili. Ili kufikia lengo hilo, makala hii imegawanywa katika sehemu kuu tano. Sehemu ya kwanza ni utangulizi ambao unaonesha lengo la makala hii na data zake zilizokusanywa kutoka katika fasihi simulizi na andishi ya Kiswahili. Sehemu ya pili inafafanua Nadharia ya Uhistoria Mpya iliyotumika katika makala haya. Sehemu ya tatu inajadili historia ya uhusiano wa China na Afrika Mashariki, vipindi ulivyopitia na nyanja zake kwa jumla. Sehemu ya nne ambayo ndiyo kiini cha makala haya, inaeleza uhusiano wa China na Afrika Mashariki kupitia tanzu za fasihi ya Kiswahili. Sehemu ya tano ni hitimisho ambalo linaelezea kwa muhtasari matokeo ya uchunguzi wa makala hii.

 

http://doi.org/10.56279/jk.v85i1.14 

Author Biography

Wael N.I. Othman, Chuo Kikuu cha Al-Azhar

Profesa

Published

2023-04-03

How to Cite

Othman, W. N. (2023). Uhusiano wa China na Afrika Mashariki kama Ilivyobainishwa katika Fasihi ya Kiswahili. Kiswahili, 85(2). Retrieved from http://elearning.ucc.co.tz/index.php/kiswahili/article/view/5628

Issue

Section

Articles